Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 12.16
Bible en Swahili de l’est


Règne de Joas sur Juda

1 Katika mwaka wa saba wa Yehu, Yoashi alianza kutawala; akatawala miaka arobaini huko Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Sibia wa Beer-sheba.
2 Rois 11.1-11.4 2 Chroniques 24.1-24.14 2 Rois 11.21 2 Rois 9.27 1 Chroniques 3.11
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana siku zake zote Yehoyada kuhani alizomfundisha.
2 Chroniques 24.2 2 Chroniques 24.17-24.22 2 Rois 14.3 2 Chroniques 26.4 2 Chroniques 25.2
3 Ila mahali pa juu hapakuondolewa; watu wakaendelea kutoa sadaka na kufukiza uvumba katika mahali pa juu.
2 Rois 14.4 2 Rois 18.4 1 Rois 22.43 1 Rois 15.14 2 Rois 15.35
4 Yoashi akawaambia makuhani, Fedha yote ya vitu vitakatifu iliyoletwa nyumbani mwa Bwana, fedha ya matumizi, fedha ya watu kadiri alivyoandikiwa kila mtu, na fedha yote iliyoletwa kama mtu ye yote aonavyo moyoni mwake kuileta nyumbani mwa Bwana,
2 Rois 22.4 Exode 35.5 Exode 35.29 1 Chroniques 29.3-29.9 Exode 30.12-30.16
5 makuhani na waitwae, kila mtu kwa hao awajuao; nao watatengeneza palipobomoka nyumbani, kila mahali palipoonekana pamebomoka.
Esaïe 58.12 2 Chroniques 24.7 2 Rois 12.12 1 Rois 11.27 2 Rois 22.5-22.6
6 Lakini ikawa, mwaka wa ishirini na tatu wa mfalme Yoashi, makuhani walikuwa hawajatengeneza mabomoko ya nyumba.
Philippiens 2.21 Malachie 1.10 1 Samuel 2.29-2.30 2 Chroniques 29.34 1 Pierre 5.2
7 Ndipo mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani, na makuhani wengine, akawauliza, Mbona hamtengenezi mabomoko ya nyumba? Basi sasa msipokee tena fedha kwa hao mwajuao, lakini itoeni kwa ajili ya mabomoko ya nyumba.
1 Chroniques 21.3 2 Rois 12.2 2 Chroniques 24.5-24.14 2 Chroniques 24.16 2 Rois 11.4
8 Nao makuhani wakakubali kwamba wasipokee fedha kwa watu, wala wasitengeneze mabomoko ya nyumba.
9 Lakini Yehoyada kuhani akatwaa kasha, akatoboa tundu katika kifuniko chake, akaliweka karibu na madhabahu, upande wa kuume mtu aingiapo nyumbani mwa Bwana; na makuhani, waliolinda mlangoni, wakatia ndani yake fedha yote iliyoletwa nyumbani mwa Bwana.
Marc 12.41 Jérémie 35.4 Psaumes 84.10 Luc 21.1 1 Chroniques 15.24
10 Ikawa, walipoona ya kuwa fedha nyingi imo kashani, karani wa mfalme akapanda na kuhani mkuu, wakaifunga mifukoni, wakaihesabu fedha iliyoonekana nyumbani mwa Bwana.
2 Samuel 8.17 2 Rois 19.2 2 Rois 22.12 2 Samuel 20.25 2 Rois 5.23
11 Na fedha iliyopimwa wakawapa mikononi wale waliofanya kazi, walioisimamia nyumba ya Bwana; na hao wakawatolea maseremala na wajenzi walioifanya kazi katika nyumba ya Bwana,
2 Rois 22.5-22.6 2 Chroniques 34.9-34.11 2 Chroniques 24.11-24.12
12 na hao waashi, na wakata mawe, tena kununua miti na mawe ya kuchongwa, ili kuyatengeneza mabomoko ya nyumba ya Bwana, tena kwa gharama zote za kuitengeneza nyumba.
2 Rois 22.5-22.6 1 Rois 5.17-5.18 Esdras 3.7 Esdras 5.8 Luc 21.5
13 Lakini havikufanywa kwa nyumba ya Bwana vikombe vya fedha, wala makasi, wala mabakuli, wala panda, wala vyombo vyo vyote vya dhahabu, wala vyombo vya fedha, kwa hiyo fedha iliyoletwa nyumbani mwa Bwana;
2 Chroniques 24.14 1 Rois 7.48-7.50 Nombres 10.2 Nombres 7.13-7.14 Esdras 1.9-1.11
14 kwa sababu hiyo fedha waliwapa watenda kazi, wakaitengeneza kwayo nyumba ya Bwana.
15 Walakini hawakufanya hesabu na hao watu, waliokabidhiwa fedha hiyo ili wawape watenda kazi; kwa kuwa walitenda kwa uaminifu.
2 Rois 22.7 Matthieu 24.45 Néhémie 7.2 3 Jean 1.5 Luc 16.1
16 Lakini fedha ya matoleo ya kosa, na fedha ya matoleo ya dhambi, haikuletwa nyumbani mwa Bwana; hiyo ilikuwa ya makuhani wenyewe.
Lévitique 7.7 Lévitique 5.15-5.18 Lévitique 4.29 Lévitique 4.24 Nombres 5.8-5.10
17 Ndipo akakwea Hazaeli mfalme wa Shamu akapigana na Gathi, akautwaa; Hazaeli akaelekeza uso ili akwee kwenda Yerusalemu.
2 Chroniques 24.23-24.24 2 Rois 8.12-8.15 Luc 9.51 1 Chroniques 18.1 Jérémie 42.15
18 Yoashi mfalme wa Yuda akavitwaa vyote alivyoviweka wakfu Yehoshafati, na Yehoramu, na Ahazia, baba zake, wafalme wa Yuda, navyo vyote alivyoweka wakfu mwenyewe, na dhahabu yote iliyoonekana katika hazina za nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme, akamletea Hazaeli mfalme wa Shamu; basi akaenda zake kutoka Yerusalemu.
1 Rois 15.18 2 Rois 18.15-18.16 2 Rois 16.8 1 Rois 14.26 2 Rois 12.4
19 Basi mambo yote ya Yoashi yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
1 Rois 11.41 2 Rois 8.23 1 Rois 14.29 1 Rois 14.19
20 Nao watumishi wake wakaondoka, wakafanya fitina, wakamwua Yoashi katika nyumba ya Milo, hapo panaposhukia Sila.
2 Rois 14.5 Juges 9.6 2 Samuel 5.9 1 Rois 11.27 2 Chroniques 33.24
21 Kwa maana Yozakari mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri, watumishi wake, wakampiga, naye akafa; wakamzika pamoja na babaze mjini mwa Daudi. Na Amazia mwanawe akatawala mahali pake.
2 Rois 14.1 2 Chroniques 24.26-24.27

Cette Bible est dans le domaine public.