Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 22.15
Bible en Swahili de l’est


Cantique de délivrance de David

1 Basi Daudi akamwambia Bwana maneno ya wimbo huu, siku ile Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake zote, na mkononi mwa Sauli;
Juges 5.1 Exode 15.1 Esaïe 12.1-12.6 Psaumes 50.14 2 Samuel 22.49
2 akasema, Bwana ndiye jabali langu, na ngome yangu, na mwokozi wangu, naam, wangu;
Psaumes 31.3 Psaumes 71.3 Psaumes 144.2 Psaumes 91.2 Deutéronome 32.4
3 Mungu wa mwamba wangu, nitamwamini yeye; Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, mnara wangu, na makimbilio yangu; Mwokozi wangu, waniokoa na jeuri.
Psaumes 9.9 Genèse 15.1 Esaïe 32.2 Psaumes 46.7 Psaumes 46.11
4 Nitamwita Bwana astahiliye kusifiwa; Hivyo nitaokoka na adui zangu.
Psaumes 96.4 Psaumes 18.3 Romains 10.13 Psaumes 48.1 Apocalypse 4.11
5 Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.
Psaumes 69.14-69.15 Jonas 2.3 Apocalypse 17.15 Apocalypse 17.1 Psaumes 93.3-93.4
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka; Mitego ya mauti ikanikabili.
Psaumes 116.3 Proverbes 14.27 Actes 2.24 Proverbes 5.22 Job 36.8
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, Naam, nikamlalamikia Mungu wangu;
Psaumes 116.4 Psaumes 120.1 Psaumes 34.6 Psaumes 18.6 Psaumes 34.15-34.17
8 Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka, Misingi ya mbinguni ikasuka-suka Na kutikisika, kwa sababu alikuwa na ghadhabu.
Juges 5.4 Job 26.11 Psaumes 97.4 Psaumes 77.18 Habakuk 3.6-3.11
9 Kukapanda moshi kutoka puani mwake, Moto ukatoka kinywani mwake ukala; Makaa yakawashwa nao.
Hébreux 12.29 Esaïe 30.27 Psaumes 18.8 Psaumes 97.3-97.5 Exode 19.18
10 Aliziinamisha mbingu akashuka; Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.
1 Rois 8.12 Psaumes 97.2 Psaumes 144.5 Exode 20.21 Esaïe 64.1-64.3
11 Akapanda juu ya kerubi akaruka; Naam, alionekana juu ya mabawa ya upepo.
Psaumes 104.3 Psaumes 18.10 Hébreux 1.14 Ezéchiel 10.2-10.14 Psaumes 99.1
12 Akafanya giza hema zake za kumzunguka, Makusanyiko ya maji, mawingu makuu ya mbinguni.
2 Samuel 22.10 Psaumes 97.2 Job 36.29 Psaumes 18.11-18.12 Psaumes 27.5
13 Toka mwangaza uliokuwa mbele zake Makaa ya moto yakawashwa.
2 Samuel 22.9
14 Bwana alipiga radi toka mbinguni, Naye Aliye juu akaitoa sauti yake.
Job 37.2-37.5 1 Samuel 2.10 Esaïe 30.30 1 Samuel 12.17-12.18 Apocalypse 11.19
15 Akapiga mishale, akawatawanya; Umeme, naye akawatapanya.
Deutéronome 32.23 Habakuk 3.11 Josué 10.10 Psaumes 45.5 Psaumes 18.14
16 Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari, Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa, Kwa kukemea kwake Bwana, Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.
Nahum 1.4 Exode 15.8-15.10 Matthieu 8.26-8.27 Exode 14.21-14.27 Psaumes 114.3-114.7
17 Alipeleka kutoka juu, akanishika; Akanitoa katika maji mengi;
Psaumes 144.7 Apocalypse 17.15 Psaumes 32.6 Lamentations 3.54 Esaïe 43.2
18 Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu, Na wale walionichukia; Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.
2 Corinthiens 1.10 Psaumes 56.9 2 Timothée 4.17 Psaumes 3.7 2 Samuel 22.1
19 Walinikabili siku ya msiba wangu; Lakini Bwana alikuwa tegemeo langu.
Psaumes 71.20-71.21 1 Samuel 19.11-19.17 Psaumes 118.10-118.13 Psaumes 23.4 1 Samuel 23.26-23.27
20 Akanitoa akanipeleka panapo nafasi; Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
Psaumes 31.8 2 Samuel 15.26 Psaumes 118.5 Psaumes 22.8 Osée 4.16
21 Bwana alinitendea sawasawa na haki yangu; Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.
1 Samuel 26.23 Psaumes 24.4 1 Rois 8.32 Psaumes 7.8 Psaumes 19.11
22 Maana nimezishika njia za Bwana, Wala sikumwasi Mungu wangu.
Proverbes 8.32 Genèse 18.19 Psaumes 128.1 2 Corinthiens 1.12 Hébreux 10.38-10.39
23 Maana hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu; Na kwa habari za amri zake, sikuziacha.
Psaumes 119.102 Psaumes 119.30 Deutéronome 8.11 Psaumes 19.8-19.9 Deutéronome 7.12
24 Nami nalikuwa mkamilifu kwake, Nikajilinda na uovu wangu.
Genèse 6.9 Job 1.1 Genèse 17.1 Jean 1.47 Hébreux 12.1
25 Basi Bwana amenilipa sawasawa na haki yangu; Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.
2 Samuel 22.21 Romains 2.7-2.8 2 Corinthiens 5.10 Proverbes 5.21 Esaïe 3.10
26 Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;
Matthieu 5.7 Jacques 2.13
27 Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu; Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.
Matthieu 5.8 Psaumes 125.5 Exode 18.11 Psaumes 18.26 Esaïe 45.9
28 Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa; Ila macho yako ni juu ya wenye kiburi, uwadhili.
Psaumes 72.12-72.13 Esaïe 5.15 Esaïe 2.17 Esaïe 2.11-2.12 Exode 3.7-3.8
29 Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee Bwana; Na Bwana ataniangazia giza langu.
Psaumes 27.1 Job 29.3 Psaumes 84.11 Esaïe 50.10 2 Samuel 21.17
30 Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi; Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.
Psaumes 18.29 Philippiens 4.13 Romains 8.37 Psaumes 118.10-118.12
31 Mungu njia yake ni kamilifu; Ahadi ya Bwana imehakikishwa; Yeye ndiye ngao yao Wote wanaomkimbilia.
Proverbes 30.5 Matthieu 5.48 Deutéronome 32.4 Psaumes 12.6 2 Samuel 22.3
32 Maana ni nani aliye Mungu, ila Bwana? Ni nani aliye mwamba, ila Mungu wetu?
1 Samuel 2.2 Esaïe 44.8 Esaïe 44.6 Deutéronome 32.31 2 Samuel 22.2-22.3
33 Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu; Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.
Philippiens 4.13 Job 22.3 Exode 15.2 Psaumes 101.6 2 Corinthiens 12.9
34 Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu; Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.
Deutéronome 32.13 Habakuk 3.19 Esaïe 58.14 2 Samuel 2.18 Esaïe 33.16
35 Ananifundisha mikono yangu vita; Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba.
Psaumes 144.1 Psaumes 18.33-18.34 Ezéchiel 39.9-39.10 Psaumes 46.9 Ezéchiel 39.3
36 Nawe umenipa ngao ya wokovu wako; Na unyenyekevu wako umenikuza.
Ephésiens 6.16 Psaumes 115.14 Psaumes 84.11 Genèse 22.17 Psaumes 18.35
37 Umezifanyizia nafasi hatua zangu, Wala miguu yangu haikuteleza.
Proverbes 4.12 1 Samuel 2.9 Psaumes 17.5 Psaumes 18.36 Psaumes 94.18
38 Nimewafuatia adui zangu, na kuwaangamiza; Wala sikurudi nyuma hata walipokomeshwa.
2 Samuel 5.18-5.25 2 Samuel 8.13-8.14 Romains 8.37 2 Samuel 8.1-8.2 2 Samuel 10.14
39 Nami nimewakomesha na kuwapiga-piga wasiweze kusimama; Naam, wameanguka chini ya miguu yangu.
Malachie 4.3 Psaumes 18.37 Psaumes 110.5-110.6 Psaumes 118.10-118.12 Malachie 4.1
40 Maana umenifunga mshipi wa nguvu kwa vita; Umenitiishia chini yangu walioniondokea.
Psaumes 44.5 Colossiens 1.11 Psaumes 18.39 Psaumes 18.32 Apocalypse 5.9
41 Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo, Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.
Exode 23.27 Josué 10.24 Genèse 49.8 Luc 19.27 Psaumes 21.8-21.9
42 Walitazama, lakini hakuna wa kuokoa; Walimwita Bwana, lakini hakuwajibu.
Esaïe 1.15 1 Samuel 28.6 Proverbes 1.28 Michée 3.4 Matthieu 7.22-7.23
43 Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi, Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.
Michée 7.10 Esaïe 10.6 2 Rois 13.7 Zacharie 10.5 Psaumes 18.42
44 Nawe umeniokoa na mashindano ya watu wangu; Umenihifadhi niwe kichwa cha mataifa; Watu nisiowajua watanitumikia.
Esaïe 55.5 2 Samuel 8.1-8.14 2 Samuel 3.1 2 Samuel 19.9 2 Samuel 19.14
45 Wageni watanijia wakinyenyekea; Kwa kusikia tu habari zangu, Mara watanitii.
Psaumes 66.3 Psaumes 81.15 Actes 8.21-8.23 Actes 8.13 Deutéronome 33.29
46 Wageni nao watatepetea, Watatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Michée 7.17 Esaïe 64.6 Amos 9.3 Esaïe 2.19 Jacques 1.11
47 Bwana ndiye aliye hai; Na ahimidiwe mwamba wangu; Na atukuzwe Mungu wa mwamba wa wokovu wangu;
Psaumes 89.26 Deutéronome 32.39-32.40 Job 19.25 2 Samuel 22.3 Luc 1.47
48 Naam, Mungu anipatiaye kisasi, Na kuwatweza watu chini yangu,
Psaumes 144.2 Psaumes 94.1 Psaumes 110.1 1 Samuel 25.39 1 Samuel 25.30
49 Na kunileta nje nitoke kwa adui zangu; Naam, waniinua juu yao walioniinukia; Waniponya na mtu wa jeuri.
Psaumes 140.1 2 Samuel 7.8-7.9 Psaumes 140.4 1 Samuel 2.8 Psaumes 18.48
50 Basi, Bwana, nitakushukuru kati ya mataifa, Nami nitaliimbia jina lako.
Romains 15.9 Psaumes 146.1-146.2 Psaumes 18.49 Psaumes 145.1-145.2 Esaïe 12.1-12.6
51 Ampa mfalme wake wokovu mkuu; Amfanyia fadhili masihi wake Daudi na mzao wake ,hata milele.
Psaumes 144.10 Psaumes 89.20 2 Samuel 7.12-7.13 Psaumes 18.50 Psaumes 89.29

Cette Bible est dans le domaine public.